Sifa Za Bwana Kwa Matendo Ya Ajabu
1 MsifuniBwana.
NitamtukuzaBwanakwa moyo wangu wote,
katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 Kazi zaBwanani kuu,
wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu,
haki yake hudumu daima.
4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe,
Bwanani mwenye neema na huruma.
5 Huwapa chakula wale wanaomcha,
hulikumbuka agano lake milele.
6 Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake,
akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki,
mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 Zinadumu milele na milele,
zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 Aliwapa watu wake ukombozi,
aliamuru agano lake milele:
jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 KumchaBwanandicho chanzo cha hekima,
wote wanaozifuata amri zake wana busara.
Sifa zake zadumu milele.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/111-fcbaf92f4ba0a7f3ecc7034f23b9cdb2.mp3?version_id=1627—