Categories
Zaburi

Zaburi 110

Bwana Na Mfalme Wake Mteule

Zaburi ya Daudi.

1 Bwanaamwambia Bwana wangu:

“Keti mkono wangu wa kuume,

mpaka nitakapowafanya adui zako

kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”

2 Bwanaataeneza fimbo yako ya utawala yenye nguvu kutoka Sayuni;

utatawala katikati ya adui zako.

3 Askari wako watajitolea kwa hiari

katika siku yako ya vita.

Ukiwa umevikwa fahari takatifu,

kutoka tumbo la mapambazuko

utapokea umande wa ujana wako.

4 Bwanaameapa,

naye hatabadilisha mawazo yake:

“Wewe ni kuhani milele,

kwa mfano wa Melkizedeki.”

5 Bwana yuko mkono wako wa kuume,

atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.

6 Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga

na kuwaponda watawala wa dunia nzima.

7 Atakunywa maji katika kijito kando ya njia,

kwa hiyo atainua kichwa chake juu.

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/110-8f324b599490c012590b4eb9baf7390b.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *