Kumtumaini Bwana
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 KwaBwananinakimbilia,
unawezaje basi kuniambia:
“Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao,
huweka mishale kwenye uzi wake,
wakiwa gizani ili kuwapiga
wale wanyofu wa moyo.
3 Wakati misingi imeharibiwa,
mwenye haki anaweza kufanya nini?”
4 Bwanayuko ndani ya Hekalu lake takatifu;
Bwanayuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.
Huwaangalia wana wa watu,
macho yake yanawajaribu.
5 Bwanahuwajaribu wenye haki,
lakini waovu na wanaopenda jeuri,
nafsi yake huwachukia.
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali
na kiberiti kinachowaka,
upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
7 Kwa kuwaBwanani mwenye haki,
yeye hupenda haki.
Wanyofu watauona uso wake.
—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/PSA/11-5c07d8f7f91202ea2f0e5f2cfada8510.mp3?version_id=1627—