Categories
Yuda

Yuda Utangulizi

Utangulizi

Mwandishi wa waraka huu ni Yuda, aliyekuwa nduguye Yakobo, yule aliyekuwa msimamizi wa baraza la Yerusalemu, na mwandishi wa waraka wa Yakobo. Alikuwa ndugu wa Yesu kwa kuzaliwa na Maria (

Marko 6:3

).

Muktadha wa waraka huu na yale yaliyomo kwenye waraka wa 2 Petro yanaashiria kuwa Yuda alikuwa amehamasishwa na ujumbe wa Petro. Yuda anaonyesha kuwa alikusudia kuandika kuhusu wokovu, lakini akabadili nasaha zake ili kukemea mtazamo wa watu fulani wenye tabia mbaya, waliokuwa wakizunguka miongoni mwa waumini wakipotosha neema ya Mungu.

Mwandishi

Yuda, ndugu yake Yesu.

Kusudi

Kukumbusha kanisa umuhimu wa kuitetea imani, na kulionya juu ya watu waovu wanaozunguka miongoni mwao wakipotosha imani.

Mahali

Hapajulikani.

Tarehe

Kama 65 B.K.

Wahusika Wakuu

Yuda, Yakobo, na Yesu.

Wazo Kuu

Yuda anasisitiza umuhimu wa kuitetea imani. Wapotovu na wazushi ni lazima waonyeshwe wazi kwamba sio wa kweli. Yuda anaonya kwamba hukumu ya Mungu itawafikia wale waliopotoka katika imani, kama vile ilivyowafikia Kaini, Kora, na Balaamu.

Mambo Muhimu

Kuweka wazi walimu wa uongo na kuwakemea vikali. Anamalizia ujumbe wake kwa kuonyesha wazi kwamba Mungu anaweza kumlinda muumini, ili aweze kuishi maisha yaliyonyooka, na hatimaye kufika mbele ya Mungu bila lawama wala mawaa.

Mgawanyo

Utangulizi (

1-4

)

Maonyo dhidi ya uongo (

5-16

)

Adibisho na hitimisho (

17-25

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *