Categories
Yona

Yona Utangulizi

Utangulizi

Yona maana yake ni “Hua.” Kitabu hiki kinaelezea yale yaliyomtukia kama mjumbe wa Mungu. Yona alikuwa ameagizwa na Mungu aende akawaonye watu wa Ninawi juu ya hukumu iliyokuwa inakuja. Alijaribu kumkimbia Mungu na kuelekea Tarshishi, upande wa magharibi wa Israeli ilhali Ninawi ilikuwa kaskazini mashariki. Yona alipotupwa baharini alimezwa na nyangumi ambaye alimrudisha mpaka pwani ya mashariki ya Bahari ya Kati (Mediterania). Hatimaye alikwenda Ninawi na kuwaonya watu kuhusu hukumu ya Mungu. Alivunjika moyo watu wa Ninawi walipotubu na Mungu akaonyesha rehema zake kwa kughairi na kuahirisha siku ya hukumu.

Mwandishi

Yona mwana wa Amitai.

Kusudi

Kuonyesha ukubwa wa neema ya Mungu, na kuwa wokovu ni kwa watu wote.

Mahali

Israeli, Bahari ya Kati (Mediterania) na Ninawi.

Tarehe

Kati ya 785–760 K.K.

Wahusika Wakuu

Yona, nahodha wa meli na mabaharia, mfalme wa Ninawi, na Waninawi wote.

Wazo Kuu

Watu wanaposikia neno la Mungu, wanapoamini na kutubu, Mungu huonyesha rehema na kufuta hukumu iliyokuwa inawakabili. Mungu hapendi mtu yeyote aangamie, bali wafikie toba.

Mambo Muhimu

Rehema za Mungu na upendo wa Mungu kwa watu wote.

Mgawanyo

Yona anamtoroka Mungu (

1:1-17

)

Sala ya Yona na kuokolewa (

2:1-10

).

Yona aenda Ninawi (

3:1-10

)

Yona amkasirikia Mungu kwa sababu ya rehema zake (

4:1-11

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *