Categories
Yoeli

Yoeli Utangulizi

Utangulizi

Yoeli mwana wa Pethueli maana ya jina lake ni “Bwana ni Mungu.” Nyingi ya kumbukumbu zake katika hiki kitabu na huduma yake hekaluni zinaonyesha kwamba alikuwa nabii aliyetumwa kwa Yuda na Yerusalemu. Kutokana na huduma yake, wengi wamemdhania kuwa nabii wa “kikuhani” (linganisha

Yer 28:1

5

) aliyenena neno la kweli la Bwana.

Tukio la unabii wa Yoeli lilikuwa pigo kubwa la nzige waliokula kila jani bichi na hata magome ya miti na mizizi. Akiwaonya watu wamgeukie

Bwana

kwa njia ya toba, Yoeli anatangaza kwamba “siku ya

Bwana

” inakuja na italeta hukumu kubwa. Kabla hiyo hukumu haijakuja, Mungu atatuma Roho wake ili kuleta baraka. Yoeli anaelezea kwa undani kuhusu kundi la nzige walioshambulia Palestina. Katika tukio hili aliona ishara ya hukumu ya mwisho na akawaonya watu watubu na kumrudia Mungu.

Mwandishi

Yoeli mwana wa Pethueli.

Kusudi

Kuionya Yuda juu ya hukumu ya Mungu iliyokuwa karibu kwa sababu ya dhambi zake, na kuwahimiza watu wamrudie Mungu.

Mahali

Yerusalemu.

Tarehe

Miaka 835–796 K.K.

Wahusika Wakuu

Yoeli na watu wa Yuda.

Wazo Kuu

Toba husababisha Mungu kughairi mabaya aliyoyakusudia, na badala yake kuleta baraka.

Mambo Muhimu

Pigo la nzige, kuwaonya watu watubu, na tumaini kwa watu wa Mungu.

Mgawanyo

Kuvamiwa na nzige (

1:1-12

)

Wito wa kutubu (

1:12-20

)

Maonyo na baraka za Mungu (

2:1-32

)

Hukumu ya Mungu ya mwisho, na sheria (

3:1-12

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *