Categories
Yeremia

Yeremia 45

Ujumbe Kwa Baruku

1 Hili ndilo nabii Yeremia alilomwambia Baruku mwana wa Neria katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, baada ya Baruku kuandika katika kitabu maneno ambayo yalitoka kinywani mwa Yeremia wakati ule:

2 “Hili ndiloBwana, Mungu wa Israeli, akuambialo wewe Baruku:

3 Ulisema, ‘Ole wangu!Bwanaameongeza huzuni juu ya maumivu yangu, nimechoka kwa kulia kwa uchungu wala sipati pumziko.’ ”

4 Bwanaakasema, “Mwambie hivi: ‘Hili ndilo asemaloBwana: Nitakibomoa kile nilichokijenga, na kungʼoa kile nilichokipanda katika nchi yote.

5 Je, utajitafutia mambo makubwa kwa ajili yako mwenyewe? Usiyatafute hayo. Kwa kuwa nitaleta maangamizi juu ya watu wote, asemaBwana, lakini popote utakapokwenda, nitayaokoa maisha yako.’ ”

—https://api-cdn.youversionapi.com/audio-bible-youversionapi/337/32k/JER/45-ec89824bdbfc3cb8636fd7a64eb5df53.mp3?version_id=1627—

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *