Categories
Wimbo

Wimbo Utangulizi

Utangulizi

Kitabu hiki huitwa “Wimbo wa Nyimbo” yaani “Wimbo Mzuri Kupita Zote,” na ni tafsiri ya moja kwa moja kutoka kwa Kiebrania “Shir Hash-Shirim,” na Kiyunani “Asma Asmaton.” Nyongeza “Asher li-Shelomoth,” ambayo imetafsiriwa “Wimbo wa Solomoni,” ndiyo chimbuko ya jina linalotumika kwa kawaida katika Kiingereza.

Mwandishi

Inadhaniwa kuwa mwandishi wa kitabu hiki ni Solomoni.

Kusudi

Kusudi la kitabu hiki ni kuthibitisha utakatifu wa ndoa, na kuonyesha picha ya upendo wa Mungu kwa watu wake.

Mahali

Bustani ya mwanamke Mshulami na jumba la kifalme.

Tarehe

Hakuna uhakika wa tarehe ya kuandikwa kwa kitabu hiki.

Wahusika Wakuu

Mfalme Solomoni, Mwanamke Mshulami, na marafiki.

Wazo Kuu

Watu wengine wanafananishia Wimbo Ulio Bora na upendo wa Kristo kwa kanisa lake. Lakini vinavyokubalika zaidi ni kwamba Wimbo Ulio Bora ni mkusanyo wa mashairi kati ya wawili wapendanao. Ni picha nzuri ya upendo wa mume na mke katika ndoa.

Mambo Muhimu

Mambo yanayohusu upendo na ndoa.

Mgawanyo

Bibi arusi na bwana arusi (

1:1–2:7

)

Sifa za mpenzi wake (

2:8–3:5

)

Kumsifu bibi arusi (

3:6–5:1

)

Upendo wenye msukosuko (

5:2–7:9

)

Urafiki ambao haujavunjika (

7:10–8:14

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *