Categories
Wagalatia

Wagalatia Utangulizi

Utangulizi

Paulo aliandika waraka huu katika safari yake ya kwanza ya kueneza Injili. Baada yake kuondoka Galatia, waumini Wayahudi walifika huko, nao wakaanza kusisitiza kwamba lazima watu wa Mataifa walioamini kwanza watimize Sheria ya Mose ili wapate kuokoka. Paulo aliandika kupinga mafundisho hayo, akionyesha jinsi Abrahamu, ambaye aliishi miaka 400 kabla ya Sheria ya Mose kutolewa, alivyookolewa kwa imani. Alionyesha kwamba kama vile Sheria haingeweza kumwokoa mtu, basi hakuna mtu angeweza kuwa mkamilifu kwa kujitahidi kwa uwezo wake mwenyewe kuitimiza Sheria.

Mwandishi

Mtume Paulo.

Kusudi

Kukataa mafundisho ya kuwa muumini wa Mataifa ni lazima atii sheria za Kiyahudi ndio aokolewe.

Wazo Kuu

Paulo anatetea kwa bidii kweli ya Injili ambayo kiini chake ni kwamba, “Mtu anaokolewa kwa neema ya Mungu kwa kumwamini Kristo.”

Mambo Muhimu

Paulo anasisitiza uhalali wa Injili, ubora wa Injili, na uhuru wa Injili.

Mahali

Antiokia.

Tarehe

Kama 49 B.K.

Wahusika Wakuu

Paulo, Tito, Barnaba, Petro, na walimu wa uongo.

Mgawanyo

Paulo atetea Injili na mamlaka yake kama mtume (

1:1–2:21

)

Kuwekwa huru kutokana na Sheria (

3:1-24

)

Ukuu wa Injili juu ya Sheria (

3:25–4:31

)

Uhuru wa Mkristo (

5:1-26

)

Mawaidha kuhusu mwenendo wa Mkristo (

6:1-18

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *