Categories
Wafilipi

Wafilipi Utangulizi

Utangulizi

Paulo alitembelea mji wa Filipi katika safari yake ya pili ya kitume, kutokana na maono aliyoyapata akiwa Troa kumwelezea aelekee Makedonia. Filipi hapakuwa na Sinagogi kwa sababu ya idadi ndogo ya Wayahudi. Kanisa la Filipi lilimpelekea Paulo msaada kupitia kwa Epafrodito. Pia alitumia nafasi hiyo kuelezea matatizo aliyopata huko Rumi. Waumini wote waliambiwa wawe na malengo ya juu kabisa katika maisha yao ya Kikristo, kwa maana Mungu angewatimizia mahitaji yao yote katika maisha. Paulo aliwakazia kufurahi nyakati zote.

Mwandishi

Mtume Paulo.

Kusudi

Kuwashukuru rafiki zake wapendwa waliokuwa wamempelekea msaada kwa ajili ya mahitaji yake. Kuwatia Wafilipi moyo na kuwataka kusimama imara, akiwahimiza wawe na unyenyekevu kama aliokuwa nao Kristo, na pia wawe na umoja.

Mahali

Rumi.

Tarehe

Kama mwaka wa 61 B.K.

Wahusika Wakuu

Paulo, Timotheo, Epafrodito, Euodia na Sintike.

Wazo Kuu

Paulo alisisitiza kuhusu furaha ya muumini katika Kristo.

Mambo Muhimu

Paulo anaagiza waumini kukataa kabisa mafundisho ya uongo na kuwahimiza wafurahi nyakati zote.

Mgawanyo

Paulo na matatizo yake huko Rumi (

1:1-30

)

Mfano wa utii wa Yesu (

2:1-30

)

Mafundisho kuhusu mwenendo wa Mkristo (

3:1-21

)

Amani ya Mungu, na jinsi Mungu anavyowatimizia waumini mahitaji yao (

4:1-23

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *