Categories
Sefania

Sefania Utangulizi

Utangulizi

Maana ya Sefania ni “Aliyefichwa na Yehova.” Alikuwa wa ukoo wa Hezekia, mfalme wa Yuda. Nabii Sefania alihudumu wakati wa utawala wa Mfalme Yosia. Sefania alionya kwamba siku ya Bwana ingeleta hukumu kwa Yuda pamoja na Yerusalemu, hivyo akawashauri Wayahudi kumrudia Mungu. Uvamizi wa kuteka Yuda ulikuwa unakuja kutoka kaskazini, nao ungekumba pia mataifa yaliyowazunguka. Ingawa hukumu ya Yuda imeainishwa, ahadi ya kufanywa upya ni yakini. Mataifa yatahukumiwa na kutiishwa na mfalme wa Israeli, atakayetawala kutoka Sayuni.

Mwandishi

Sefania.

Kusudi

Kuwaonya watu wa Yuda waepukane na kuabudu sanamu na wamrudie Mungu wao.

Mahali

Yerusalemu.

Tarehe

Kati ya 640–621 K.K.

Wahusika Wakuu

Sefania, na watu wa Yuda.

Wazo Kuu

Sefania aliwapa watu matumaini kwamba Mungu angewarudisha watu wake nyumbani.

Mambo Muhimu

Hukumu juu ya Yuda na mataifa ya Wafilisti, Amoni na Moabu. Yerusalemu pia inatajwa kwa siku zijazo.

Mgawanyo

Kutangazwa kwa hukumu ya Mungu (

1:1–2:3

)

Hukumu dhidi ya mataifa (

2:4-15

)

Maisha ya baadaye ya Yerusalemu (

3:1-20

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *