Categories
Nahumu

Nahumu Utangulizi

Utangulizi

Nahumu ambaye jina lake linamaanisha “Faraja” alikuwa mwenyeji wa Elikoshi. Alihudumu wakati mmoja na Sefania, Yeremia na Habakuki. Katika ujumbe wake alizungumzia kuanguka kwa Thebesi mwaka wa 663 K.K. na kuanguka kwa Ninawi mnamo mwaka wa 612 K.K. Nahumu anaeleza kwa wazi juu ya uonevu na udhalimu wa kikatili wa Ashuru, na jinsi walivyosonga mbele na kushinda taifa moja baada ya lingine.

Ukatili huo usiokuwa na chembe cha huruma usingeweza kuvumiliwa na Mungu mwenye haki aliye mtakatifu pasipo kikomo. Katika unabii huu Nahumu anaelezea vizuri na kuonyesha kuzingirwa na kuanguka kwa Ninawi kuwa ndio mwisho wa huu ufalme wenye nguvu wa Ashuru, ambao ndio ulikuwa unakalia sehemu zenye rutuba kwa zaidi ya karne nzima. Kwa nasaha fupi kwa watu wa Yuda, Nahumu anawashauri watu wake kuzitii sikukuu zao za kidini, kwa kuwa Waashuru wasingeliishambulia tena Yerusalemu.

Mwandishi

Nahumu.

Kusudi

Kutamka hukumu ya Mungu dhidi ya Waashuru na kuwafariji Yuda.

Tarehe

Kati ya 663–612 K.K.

Mahali

Ninawi.

Wahusika Wakuu

Waninawi.

Wazo Kuu

Yehova ni Mungu mwenye wivu ambaye mapatilizo yake kwa hakika lazima yawapate adui zake, lakini yeye ni ngome kwa wale wanaomtumaini.

Mambo Muhimu

Nahumu anaeleza kukaribia kwa hukumu ya Ninawi na jinsi itakavyokuwa kwa lugha ya wazi. Anaorodhesha kwa kifupi dhambi za Ninawi na kutamka kwamba Mungu ni mwenye haki katika hukumu zake. Anamalizia kwa kuiona hukumu iliyokamilika. Hiki ndicho kitabu cha Agano la Kale kinachotoa unabii wake waziwazi juu ya ukatili wa Waashuru.

Mgawanyo

Hasira ya Mungu dhidi ya Ninawi (

1:1-15

)

Kuanguka kwa Ninawi (

2:1-13

)

Ukiwa kwa Ninawi (

3:1-19

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *