Categories
Malaki

Malaki Utangulizi

Utangulizi

Malaki maana yake ni “Mjumbe Wangu” au “Mjumbe wa

Bwana

.” Malaki aliishi baada ya ujenzi wa Hekalu la pili kumalizika. Maisha ya uchaji wa Mungu ya Wayahudi yalikuwa mabaya. Walikuwa wamekengeuka, wakawaoa wanawake wa mataifa mengine, wakaacha kutoa zaka na dhabihu ambayo ni sehemu ya Mungu, hata wakawa wamemwacha Mungu, hali ambayo ilifanana sana na ile iliyokuwepo wakati wa Nehemia.

Mwandishi

Malaki.

Kusudi

Kuwahimiza watu wafanye mabadiliko thabiti ya kimsingi katika maisha yao kwa kuziacha dhambi zao ili kurejeza uhusiano wao na Mungu na kuwakumbusha upendo wa Mungu.

Mahali

Yerusalemu na Hekaluni.

Tarehe

Kama 430 K.K.

Wahusika Wakuu

Malaki, makuhani, na watu wa Yuda.

Wazo Kuu

Mungu anawapenda watu wake hata wakati wanapomwacha na kutomtii. Ana baraka nyingi anazowapa wale walio waaminifu kwake. Upendo wake hauna mwisho.

Mambo Muhimu

Kitabu hiki kinaonyesha kuwa Hekalu lilijengwa tena, na dhabihu na sikukuu zikarudishwa. Ufahamu wa jumla wa Sheria ulirudishwa tena na Ezra, na kurudi kwao nyuma kimaadili kulikofuatia kulitokea zaidi miongoni mwa makuhani.

Mgawanyo

Upendo wa Mungu kwa Israeli (

1:1-5

)

Israeli wamtukana Mungu (

1:6–2:16

)

Hukumu ya Mungu na ahadi yake (

2:17–4:6

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *