Categories
Hagai

Hagai Utangulizi

Utangulizi

Hagai ni moja ya vitabu vitatu vya kinabii vya Agano la Kale vilivyoandikwa baada ya uhamisho. Hagai na Zekaria ndio waliowatia moyo watu waliorudi kutoka uhamishoni kujenga upya Hekalu baada ya Mfalme Dario kupitisha amri kuwaruhusu Wayahudi kurudi Yerusalemu.

Kundi la kwanza la Wayahudi liliporudi Yerusalemu liliweka msingi wa Hekalu jipya wakiwa na furaha na matumaini makubwa. Hata hivyo, Wasamaria na majirani wengine walipinga ujenzi huo kwa nguvu nyingi na kuwakatisha tamaa wafanyakazi, na hata kuufanya ujenzi huo usimame. Watu wakageukia ujenzi wa nyumba zao wenyewe. Ujumbe wa Hagai ulikuwa kwamba ni wakati wa kujenga nyumba ya Mungu.

Mwandishi

Hagai.

Kusudi

Kuwahimiza watu kujenga upya Hekalu la

Bwana

, na kuwahamasisha kuyatengeneza maisha yao upya na Mungu ili waweze kupata baraka zake.

Mahali

Yerusalemu.

Tarehe

520 K.K.

Wahusika Wakuu

Hagai, Zerubabeli, Yoshua.

Wazo Kuu

Hagai aliwaambia watu kwamba utukufu wa Hekalu walilokuwa wanajenga ungekuwa mkubwa kuliko ule wa Hekalu lililotangulia, ingawaje halingekuwa imara kama la kwanza. Hili Hekalu lingekuwa bora zaidi kwa sababu Mungu angelijaza utukufu wake ndani yake.

Mambo Muhimu

Kuwaita watu kujenga upya Hekalu la Yerusalemu lililobomolewa, na ahadi ya Mungu ya kuwabariki kama wangemtii.

Mgawanyo

Wito wa kujenga Hekalu (

1:1-15

)

Matumaini ya Hekalu jipya (

2:1-9

)

Baraka zilizoahidiwa (

2:10-19

)

Ushindi wa mwisho wa Mungu (

2:20-23

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *