Categories
Filemoni

Filemoni Utangulizi

Utangulizi

Waraka huu mfupi umeainishwa na nyaraka za Waefeso, Wakolosai na Wafilipi kama mojawapo wa nyaraka Paulo alizoandika akiwa gerezani. Aliandikia Filemoni, Afia mwanamke Mkristo (ambaye huenda alikuwa mkewe Filemoni), na Arkipo, na kanisa lililokuwa likikusanyika nyumbani kwa Filemoni.

Onesimo alikuwa mtumwa aliyetoroka kutoka kwa Filemoni huko Kolosai akaenda Rumi, ambako aliokoka. Onesimo, kama mtumwa, alikuwa mali ya Filemoni kisheria.

Mwandishi

Mtume Paulo.

Kusudi

Kumhimiza Filemoni amsamehe Onesimo, mtumwa aliyemtoroka, na amkubali kama ndugu Mkristo katika imani.

Mahali

Rumi.

Tarehe

Kama mwaka wa 60 B.K.

Wahusika Wakuu

Paulo, Filemoni, na Onesimo.

Wazo Kuu

Paulo alimwandikia Filemoni kumshawishi amkubali Onesimo kurudi kwake, na amsamehe aliyomkosea.

Mambo Muhimu

Barua hii ni kielelezo cha ukarimu wa Kikristo. Paulo alishukuru kwa moyo wa ukarimu ambao tayari Filemoni alikuwa ameonyesha kwa Wakristo wenzake. Paulo kwa mamlaka yake ya kitume katika kanisa angeweza kumtaka afanye hivyo kwa Onesimo. Badala yake Paulo aliomba kwa upendo Filemoni ampokee Onesimo.

Mgawanyo

Salamu (

1-3

)

Kuhusika kwa Paulo, na upendo wake (

4-7

)

Paulo kumwombea Onesimo (

8-22

)

Kuagana (

23-25

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *