Categories
Danieli

Danieli Utangulizi

Utangulizi

Kitabu hiki kinatoa kumbukumbu za Danieli wakati wa utumishi wake wa muda mrefu katika falme za Babeli na Uajemi. Alipokuwa mateka katika jumba la mfalme huko Babeli, Danieli alipandishwa cheo na kupewa wadhifa wa juu baada ya kumwambia Nebukadneza ndoto yake na tafsiri yake. Katika mwongo wa mwisho wa maisha yake, Danieli alipata funuo kadha wa kadha kutoka kwa Mungu zilizowiana na ndoto ya Nebukadneza, zikionyesha kuinuka na kuanguka kwa falme za dunia zilizostawi, ambazo hatimaye zinafikia mwisho wake na kusimamishwa kwa ufalme wa milele. Danieli, kama Myahudi mcha Mungu aliyekuwa mwombaji na msomaji wa Maandiko, alikuwa anahusika na watu wake wa Israeli sana. Alihakikishiwa na Mungu kwamba wangefanywa imara tena.

Mwandishi

Danieli.

Kusudi

Kuelezea habari za Wayahudi waliokuwa mateka lakini wenye imani, na walioonyesha jinsi Mungu anavyoweza kuokoa wale wanaomtumaini kutokana na kusudio lolote baya, akionyesha uweza wake kwamba ndiye anayetawala mbingu na nchi, na kwamba falme zote za wanadamu ziko chini yake.

Mahali

Babeli.

Tarehe

536 K.K.

Wahusika Wakuu

Danieli, Shadraki, Meshaki, Abednego, Nebukadneza, Belshaza na Dario.

Wazo Kuu

Danieli aliandika kitabu hiki Wayahudi walipokuwa utumwani ili kuwatia moyo waendelee kumwamini Mungu ambaye anatawala historia yote.

Mambo Muhimu

Maono ya Danieli yanaonyesha mpango wa Mungu kwa vizazi vyote, pamoja na kutabiri wazi kuhusu Masiya.

Mgawanyo

Matukio wakati wa utawala wa Mfalme Nebukadneza (

1:1–4:37

)

Maandishi ukutani (

5:1-30

)

Danieli katika tundu la simba (

5:31–6:28

)

Maono wakati wa utawala wa Belshaza (

7:1–8:27

)

Ndoto ya Danieli na majuma sabini (

9:1-27

)

Mafunuo ya mwisho ya Danieli (

10:1–12:13

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *