Categories
3 Yohana

3 Yohana Utangulizi

Utangulizi

Waraka wa tatu wa Yohana uliandikiwa Gayo, ambaye alikuwa kiongozi muhimu katika kanisa. Alielekezwa kuwasaidia na kuwahudumia wale waliokuja kama wajumbe wa Mungu. Pia alipewa onyo kuhusu Deotrefe, juu ya tabia yake ya kukosa ushirikiano. Yohana alieleza tarajio lake la kuja na kushughulikia tatizo hili mwenyewe.

Mwandishi

Mtume Yohana.

Kusudi

Yohana anamwandikia Gayo akimpa onyo kuhusu Deotrefe, kwa tabia yake ya kukosa ushirikiano.

Mahali

Efeso.

Tarehe

Kama mwaka wa 90 B.K.

Wahusika Wakuu

Yohana, Gayo, Deotrefe, na Demetrio.

Wazo Kuu

Wajibu binafsi wa Gayo kuhusu watumishi wa kweli na wa uongo.

Mambo Muhimu

Yohana anamtakia Gayo kufanikiwa katika mambo yote, na pia anamwagiza asiige lililo baya bali aige lililo jema.

Mgawanyo

Salamu (

1-4

)

Kutiwa moyo kwa Gayo (

5-8

)

Kukemewa kwa Deotrefe (

9-10

)

Kusifiwa kwa Demetrio (

11-12

)

Hitimisho (

13-14

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *