Categories
2 Petro

2 Petro Utangulizi

Utangulizi

Barua hii inagusia matatizo ambayo Petro aliona yangebaki baada ya kifo chake. Aliwahimiza waumini waendelee kuijua kweli iliyo katika Injili ya Kristo. Kweli hii haikutokana na hadithi za kale, bali ilitokana na mambo waliyoyaona kwa macho. Aliwaonya kuhusu walimu wa uongo ambao wangetukuza mawazo yao wenyewe, badala ya mafundisho ya kweli ya Neno la Mungu. Hatimaye aliwakumbusha waumini kwamba Kristo atakuja siku moja kuangamiza hali ya asili ya ulimwengu huu.

Mwandishi

Mtume Petro.

Kusudi

Kuwaonya Wakristo kuhusu walimu wa uongo wanaojiingiza ndani ya kanisa, na kuwahimiza kukua katika imani yao na katika kumjua Kristo.

Mahali

Uwezekano mkubwa ni kwamba waraka huu uliandikiwa Rumi.

Tarehe

Kama mwaka wa 67 B.K.

Wahusika Wakuu

Petro na Paulo.

Wazo Kuu

Umuhimu wa kusimama imara katika imani, hata kukiwa na mafundisho mengi ya kupotosha.

Mambo Muhimu

Petro anashuhudia kwamba Mungu anataka watu waishi maisha matakatifu kwa ajili ya kukua katika kumcha Kristo. Juu ya yote, anataka wasomaji wake kukaza macho yao katika kuijua kweli ambayo inapatikana tu kwa Yesu Kristo, Bwana wetu. Kwa kumjua yeye, waumini wanapokea neema, amani, na mambo yote yapasayo uzima, na utauwa au kumcha Mungu.

Mgawanyo

Namna ya kukua kiroho (

1:1-21

)

Maonyo kuhusu walimu wa uongo (

2:1-22

)

Maagizo juu ya kuja kwake Kristo mara ya pili (

3:1-18

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *