Categories
1 Wakorintho

1 Wakorintho Utangulizi

Utangulizi

Korintho ulikuwa mji uliojengwa pwani ya Mediterania (Bahari Kuu). Mji huu ulistawi kwani ulikuwa kituo kikuu cha biashara. Ulikuwa koloni la Kirumi, ukiwavutia wakazi wa mataifa mbalimbali, wakiwemo Warumi, Wayunani na Wayahudi kutoka sehemu zilizoizunguka Bahari Kuu. Mchanganyiko huu wa wakazi ulisababisha kuharibika na kuzorota kwa maadili.

Paulo alianzisha kanisa katika mji wa Korintho katika safari yake ya pili ya kitume, akakaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na nusu. Aliondoka Korintho akifuatana na Prisila na Akila kwenda Efeso, na kutoka huko alitembelea kanisa la Yerusalemu, na baadaye akarudi Antiokia. Paulo alipokea habari kutoka kwa nyumba ya Kloe kwamba kanisa lilikuwa limegawanyika. Paulo aliona ni muhimu awaandikie waraka huu ili kujibu matatizo mengi yaliyojitokeza. Aliposhughulikia matatizo haya moja kwa moja, Paulo alifafanua misingi ya mafundisho ya Kikristo kuhusu imani na maadili.

Mwandishi

Mtume Paulo.

Kusudi

Kusahihisha makosa dhahiri katika kanisa la Korintho, na pia kuwaelimisha waumini jinsi ya kumtumikia Kristo katika jamii iliyokosa maadili.

Mahali

Efeso.

Tarehe

Kama mwaka wa 55 B.K.

Wahusika Wakuu

Paulo, Timotheo, nyumba ya Kloe, waumini wa Korintho.

Wazo Kuu

Umuhimu wa mwenendo wa Mkristo kufanana na Kristo.

Mambo Muhimu

Suluhisho za matatizo mbalimbali kama: ugomvi kanisani, uzinzi, kushtakiana, mabishano juu ya ndoa, chakula kilichotolewa kwa sanamu, hali ya Paulo kuwa mtume, matumizi mabaya ya Meza ya Bwana, ukweli kuhusu ufufuo, n.k. Lazima mwenendo wa Mkristo ufanane na ule wa Kristo; kukosa kufanya hivyo ni kumwaibisha Kristo na kanisa lake.

Mgawanyo

Salamu za Paulo (

1:1-9

)

Tatizo la mgawanyiko katika kanisa (

1:10–4:21

)

Tatizo la zinaa katika kanisa (

5:1-13

)

Tatizo la kushtakiana mahakamani (

6:1-11

)

Tatizo la uasherati (

6:12-20

)

Tatizo juu ya ndoa (

7:1-40

)

Matatizo kuhusu ibada za sanamu (

8:1–11:1

)

Matatizo kuhusu Meza ya Bwana na ibada (

11:2–14:40

)

Matatizo kuhusu ufufuo wa wafu (

15:1-58

)

Mawaidha ya mwisho (

16:1-24

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *