Categories
1 Wafalme

1 Wafalme Utangulizi

Utangulizi

Katika maandiko ya Kiebrania, vitabu vya 1 Wafalme na 2 Wafalme vilikuwa kitabu kimoja kilichoitwa “Wafalme” katika mapokeo ya Kiyahudi. Huku kutenganishwa kwa vitabu hivi kulifanywa na watafsiri wa Agano la Kale la Kiyunani “Septuagint” na kuvitambulisha kama “Kitabu cha Tatu na cha Nne cha Ufalme.” Vitabu vya Samweli na Wafalme vinaelezea historia yote kuhusu ufalme wa Israeli, vile ulivyoinuka wakati wa Samweli, na vile ulivyoanguka mikononi mwa Wababeli.

Mwandishi

Mwandishi wa kitabu hiki hajulikani, lakini mapokeo ya Kiyahudi yanasema mwandishi ni nabii Yeremia, au kikundi cha manabii.

Kusudi

Kulinganisha maisha ya wale waliomwishia Mungu na wale waliokataa kumwishia Mungu, kupitia historia ya wafalme wa Israeli na Yuda.

Mahali

Katika nchi ya Israeli.

Tarehe

Hakuna uhakika ni wakati upi hiki kitabu kiliandikwa.

Wahusika Wakuu

Daudi, Solomoni, Rehoboamu, Yeroboamu, Eliya, Ahabu na Yezebeli.

Wazo Kuu

Kugawanyika kwa Israeli kuwa falme mbili: Ufalme wa Kaskazini uliojulikana kama Israeli, ambao ulikuwa na makabila kumi, na Ufalme wa Kusini uliojulikana kama Yuda, ambao ulikuwa na makabila mawili.

Mambo Muhimu

Kifo cha Daudi, utawala wa Solomoni, kujengwa kwa Hekalu, kugawanyika kwa ufalme, na huduma ya Eliya.

Mgawanyo

Utawala wa Solomoni (

1:1–11:43

)

Rehoboamu na Yeroboamu (

12:1–14:31

)

Wafalme wa Israeli na Yuda (

15:1–16:34

)

Eliya na Ahabu (

17:1–19:21

)

Utawala wa Ahabu na Yezebeli (

20:1–22:53

).

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *